Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isiingize gharama za mita za maji kwenye vitabu vyao vya fedha badala ya kuweka pale inapounganishwa maji?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba niulize Maswali mawili madogo tu: -

(i) Je, Serikali inaweza ikatudokeza kidogo kitu gani tutegemee kutokana na huo mwongozo?

(ii) Kwa vile Serikali imeweza kutoa ruzuku kwa maunganisho ya umeme, ni nini kinazuwia kutoa ruzuku kwa maunganisho ya maji ilhali tunajua maji ni uhai?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge.

Swali la kwanza, kwa nini tunashindwa kutumia ruzuku kwenye maunganisho ya maji; hili suala naomba nilichukue tuweze kulifanyia kazi. Vilevile swali lake la kwanza naomba niwe nimelipokea nitalifanyia kazi.

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isiingize gharama za mita za maji kwenye vitabu vyao vya fedha badala ya kuweka pale inapounganishwa maji?

Supplementary Question 2

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa maji wa Njoro II, Rombo, ili kuwatua akinamama wa Rombo ndoo kichwani?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuena Bushiri, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu tunaendelea na utekelezaji wake; na kadiri tunavyopata fedha, Mheshimiwa Mbunge wewe ni shahidi, tunaendelea kupeleka fedha ili mradi huu ukamilike, kwa sababu lengo la Serikali ni kuona akina mama tunawatua ndoo kichwani.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isiingize gharama za mita za maji kwenye vitabu vyao vya fedha badala ya kuweka pale inapounganishwa maji?

Supplementary Question 3

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itakuja na bei elekezi ya kuunganisha maji nchi nzima kama ilivyo kwenye umeme?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, Profesa Ndakidemi kuhusu bei elekezi nchi nzima kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, uunganishaji wa maji tunazingatia umbali kwa sababu ya mabomba na miundombinu ambayo inatumika. Tunaangalia kutokea kwenye main line kuja kwa wewe mtumiaji pale ulipo ndivyo ambavyo gharama inakwenda.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isiingize gharama za mita za maji kwenye vitabu vyao vya fedha badala ya kuweka pale inapounganishwa maji?

Supplementary Question 4

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa wananchi wa Kibamba wanayo shukrani ya kukamilisha matenki ya Tegeta A – Goba na Mshikamano – Mbezi na mtaa Msumi hauna maji toka kupata uhuru.

Je, ni lini Serikali mtapeleka miundombinu ya kutosha, ili Mtaa huu wa Msumi, Kata ya Mbezi kupata maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtemvu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tayari Wizara tumeagiza vifaa vya kuhakikisha mradi huu na miradi yote ya eneo lile la jimbo lake tunakwenda kuikamilisha. Tayari tumeshagharamia miundombinu ya matenki makubwa kwa hiyo sasa usambazaji ndio unaofuata.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isiingize gharama za mita za maji kwenye vitabu vyao vya fedha badala ya kuweka pale inapounganishwa maji?

Supplementary Question 5

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa wananchi wengi wanalalamikia sana bili kubwa za maji pale ambapo hata hawatumii maji nikiwemo mimi, ilhali hatupo hapa Dodoma naletewa bili kubwa. Ni lini sasa Wizara ya maji italepa prepaid meters kwa wengi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, prepaid meters tunaendelea kufunga maeneo mbalimbali. Kwa hiyo naomba niseme tu Mheshimiwa Mbunge, tuendelee kuwasiliana, hata wewe ukihitaji leo unaweza ukafungiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile bili kubwa hizi za maji Waheshimiwa Wabunge pamoja na wananchi wote naomba niseme kwamba, tuangalie miundombinu yetu. Wakati fulani ni wewe mhusika peke yako ndiye unaepata bili kubwa kwa sababu, labda mita yako hapo nje inapitisha hewa au kuna tatizo la uvujaji. Kwa hiyo hizi bili kubwa naomba tutoe taarifa kwa mafundi wetu, ili tuweze kuzidhibiti.