Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 10 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 134 2023-04-19

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: -

Je, lini ujenzi wa barabara ya Kibena Stop – Lupembe hadi Madeke kwa kiwango cha lami utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Edwin Enosy Swalle, Mbunge wa Lupembe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imepanga kuanza ujenzi wa Barabara ya Kibena – Lupembe hadi Madeke yenye km 126 kwa awamu, ambapo katika mwaka wa fedha 2023/2024 itaanza ujenzi wa km 25 kwa sehemu ya kutoka Kibena hadi Nyombo. Kwa sasa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) wanaendelea kuandaa nyaraka kwa ajili ya kutangaza zabuni. Zabuni zinatarajiwa kutangazwa mwishoni mwa mwezi Juni, 2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea na ujenzi wa barabara hii kulingana na upatikanaji wa fedha hadi ikamilike yote, ahsante.