Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, lini ujenzi wa barabara ya Kibena Stop – Lupembe hadi Madeke kwa kiwango cha lami utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Kwa kuwa barabara hii ina ahadi ya muda mrefu; Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari baada ya Bunge hili kwenda Jimboni Lupembe kuwaambia wananchi juu ya ahadi hii nzuri ya Serikali?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini la pili, wananchi wa Nyombo, Kidegembye, Matembwe, Barazani, Madeke na Mfiriga nyumba zao zimewekwa X tangu mwaka 2014. Ni upi mpango wa Serikali sasa kuwalipa fidia wananchi hawa kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Edwin Enosy Swalle, Mbunge wa Lupembe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hiyo nimeshaitembelea. Na kwa kuwa tunaenda kuanza niko tayari baada ya kikao hiki cha Bunge kwenda jimboni kwa Mheshimiwa Mbunge na kuweza kuongea na wananchi, kuwaeleza nini tutakachokifanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, tulikuwa tumefanya tathmini muda na tayari tumeshamu-engage consultant kwa ajili ya kuhuisha ule uhakiki uliofanyika, ili sasa tuweze kupata taarifa za sasa kwa ajili ya kuwalipa fidia wananchi hawa ambao wote waliwekewa alama za “X” ili tuanze ujenzi.

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, lini ujenzi wa barabara ya Kibena Stop – Lupembe hadi Madeke kwa kiwango cha lami utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi, barabara inayotoka Handeni kwenda Songe na Kiteto ni siku ya pili sasa hivi haipitiki kutokana na na mvua zinazonyesha, na shughuli zote za uchumi zimesimama. Je, nini kauli ya Serikali juu ya barabara hiyo? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kigua, Mbunge wa Kilindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niwape pole wananchi wa Kilindi kwa adha wanayoipata kwa sababu ya changamoto ya mvua. Napenda nitumie nafasi hii kumuagiza Meneja wa TANROADS Mkoa wa Tanga aweze kufika maeneo yote ambayo yameathirika na kuweza kurejesha mawasiliano kwa muda, na pale ambapo changamoto itakuwa ni kubwa, basi aweze kuwasiliana na TANROADS Makao Makuu kwa ajili ya kutoa msaada mkubwa zaidi, ahsante. (Makofi)

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, lini ujenzi wa barabara ya Kibena Stop – Lupembe hadi Madeke kwa kiwango cha lami utaanza?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa upembuzi na usanifu wa barabara ya kutoka Kiranjeranje – Makangaga – Nakiu – Nanjirinji mpaka Ruangwa umekamilika, lini Serikali itajenga barabara hii kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeshafanya kama alivyosema upembuzi yakinifu, na yote hayo ni maandalizi ya kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tuna mpango wa kuijenga hii barabara kwa kiwango cha lami kuanzia Kiranjeranje hadi Ruangwa kwa kadri fedha itakavyopatikana.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, lini ujenzi wa barabara ya Kibena Stop – Lupembe hadi Madeke kwa kiwango cha lami utaanza?

Supplementary Question 4

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Naomba kumuuliza Naibu Waziri; barabara itokayo Masumbwe – Lugunga kuelekea Geita, ni lini itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maganga, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja ipo kwenye mpango wa RICE, na sasa hivi kinachoandaliwa ni document tender kwa ajili ya kuitangaza ili barabara hii iweze kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami kwa maeneo ambayo yameainishwa. Ahsante.

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, lini ujenzi wa barabara ya Kibena Stop – Lupembe hadi Madeke kwa kiwango cha lami utaanza?

Supplementary Question 5

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Bungu – Nyamisati imekuwa kilio cha muda mrefu sana kwa wananchi wa Jimbo la Kibiti; je, ni lini Serikali mtaitengeneza barabara hii katika kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Twaha Mpembenwe, Mbunge wa Kibiti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii tayari tumeshakamilisha usanifu wa kina na Serikali inaendelea kutafuta fedha ili tuweze kuijenga barabara hii yote kwa kiwango cha lami kuanzia Bungu mpaka Nyamisati. Ahsante.