Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 10 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 135 2023-04-19

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza na kukamilisha ujenzi wa barabara ya Kahama – Solwa hadi Mwanza kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christina Christopher Mnzava, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeanza ujenzi wa barabara ya Kahama – Solwa hadi Mwanza kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha ambapo kipande cha kilometa 5.65 kuanzia Kahama kuelekea Solwa pamoja na kipande cha mita 540 katika Mji Mdogo wa Bulige tayari imejengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga jumla ya shilingi milioni 750.62 kwa ajili ya ujenzi wa kilometa 1.2 kati ya Solwa na Bulige ambapo mkandarasi tayari amepatikana na amekabidhiwa mradi ili kuanza kazi. Kazi imepangwa kukamilika mwezi Septemba, 2023.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea na ujenzi wa barabara hii kwa awamu hadi kukamilika yote kulingana na upatikanaji wa fedha, ahsante.