Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza na kukamilisha ujenzi wa barabara ya Kahama – Solwa hadi Mwanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, na pia namshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali imekwisha kutenga fedha kwa mwaka wa fedha 2022/2023, je, ni lini Serikali itatoa hizo fedha ili ujenzi wa barabara uendelee?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa mkandarasi amekwisha kupatikana, na Naibu Waziri amesema kwamba Septemba ile kazi itakabidhiwa. Je, kwa kuwa mkandarasi amepatikana, ni lini ataanza hiyo kazi ili Septemba aikabidhi?(Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christina Christopher Mnzava, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mkandarasi akishakabidhiwa anachofanya ni maandalizi ya ujenzi, na kwa hiyo kwa kuwa tumeshamkabidhi, na tumekubaliana lini atamaliza kazi, mkandarasi yuko site kwa maana ya kufanya maandalizi, na mwezi Septemba tunategemea atakuwa amekamilisha hiyo kazi, na kadri Serikali itakavyoendelea kupata fedha, barabara hii tuna uhakika itakamilishwa yote, ahsante.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza na kukamilisha ujenzi wa barabara ya Kahama – Solwa hadi Mwanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, ni lini Serikali itajenga barabara kwa kiwango cha lami kuanzia Kazegunga – Mahembe – Kitanga – Kinazi mpaka Buhigwe? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Josephine Genzabuke, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja ya Mahembe – Buhigwe – Kitanga ni barabara ya mkoa ambayo tayari tumeshakamilisha kufanya usanifu na sasa tunaendelea kumlipa huyo consultant na baada ya hapo tutaanza kufanya maandalizi kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza na kukamilisha ujenzi wa barabara ya Kahama – Solwa hadi Mwanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, natambua kwamba ujenzi wa barabara ya Kisorya – Nyamswa – Bunda tayari umeshafika Nyamswa, lakini bado ujenzi unatakiwa uendelee na imekomea pale Makongoro Sekondari na inatakiwa ifike mpaka Isenye. Je, ni lini sasa ujenzi huo utaendelea kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ukishafika Nyamswa unapita kwenye T, aidha uende Mjini Musoma ama uende upande wa Nata. Na upande wa Nata ndiyo Isenye ambapo tayari kuna mkandarasi ambaye ameshajenga kutoka Makutano – Sanzate na Sanzate kwenda Nata tayari mkandarasi yuko site, nadhani kuna eneo Isenye pale tayari wameshajenga. Na wiki kama tatu nimekuwepo pale wakiwa wanaomba baada ya kuinua tuta wanahitaji kurekebisha maji pale, tumeshawarekebishia. Kwa hiyo, hiyo barabara iko kwenye ujenzi na mkandarasi yuko site (kilometa 40).

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza na kukamilisha ujenzi wa barabara ya Kahama – Solwa hadi Mwanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara ya Mbuguni inayounganisha Mikoa ya Arusha na Manyara kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pallangyo, Mbunge Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ilishaahidiwa kujengwa kwa kiwango cha lami, na tayari tumeshakamilisha usanifu. Sasa hivi Serikali inaendelea kuweka mipango ili tuweze kuijenga kwa kiwango cha lami. Naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira tuangalie kwenye bajeti tunayokwenda kuileta mbele yenu, ahsante.