Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 11 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 143 2023-04-20

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kujenga Mabwawa ya kuvuna maji ya Mvua pamoja na mifereji ya umwagiliaji ili kupunguza athari za mvua katika Mkoa wa Kilimanjaro?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Shally Josepha Raymond Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Kilimanjaro ni miongoni mwa mikoa ambayo ujenzi wa mabwawa kwa ajili ya kuvuna maji ya mvua pamoja na ujenzi wa mifereji ya umwagiliaji umeendelea ili kupunguza athari za mvua na kusaidia wakulima kujihakikishia kilimo cha mwaka mzima kupitia umwagiliaji.

Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha wa 2022/2023 Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imekamilisha mapitio ya usanifu wa ukarabati wa Bwawa la Ikuini na taratibu za kumpata mkandarasi kwa ajili ya ukarabati wa bwawa hilo unaendelea.

Mheshimiwa Spika, aidha, katika mwaka wa fedha wa 2023/2024, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imepanga kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa bwawa la Boloti na Yongoma sambamba na mifereji itakayoweza kuhudumia takribani hekta 2,000 ndani ya Wilaya ya Same.