Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Mabwawa ya kuvuna maji ya Mvua pamoja na mifereji ya umwagiliaji ili kupunguza athari za mvua katika Mkoa wa Kilimanjaro?

Supplementary Question 1

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante. Swali la kwanza, kwa kuwa katika majibu ya msingi ameitaja Boloti ambayo iko Siha na Ikuini ambayo iko Rombo tu; lakini kwenye swali langu niliuliza tambarare yote ya Mkoa wa Kilimanjaro. Sasa, ni lini wataweza kujenga mabwawa hayo Undugai katika Wilaya ya Hai, Arusha chini kule Chekereni Wilaya ya Moshi Vijijini na Kahe na kule Mwanga ikiweko na Ruvu kule Same?

Mhehimiwa Spika, swali la pili; ni lini mabwawa hayo yanayojengwa na yanayotarajiwa kukarabatiwa yatatumika kufundishia wananchi kutumia drip irrigation ambayo ni umwagiliaji wa matone ili uweze kuwa na tija kwa mazao ambayo yatakuwa yameoteshwa wakati wa ukame?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha maeneo yote yanayofaa kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa tuweze kuyafanyia kazi ili wananchi wetu waweze kulima mwaka mzima, ni muondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti yetu ambayo tutakuja kuisoma hapa tumeitengea eneo hili fedha za kutosha kuhakikisha kwamba tunapitia maeneo yote ikiwemo Mkoa wa Kilimanjaro katika maeneo ambayo ameyataja.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, teknolojia ya umwagiliaji wa matone ni kati ya teknolojia ambayo inatumika katika maeneo mengi sana hivi sasa nchini, na sisi kama Wizara ya Kilimo tunaiunga mkono. Isipokuwa tu katika Mabwawa ambayo ameyatamka teknolojia hii huwa inaendana na aina ya mazao yanayolimwa. Kwa hiyo kama mazao yanayolimwa yatakuwa yanahitaji teknolojia hii tumeshaanza, na ukienda katika Bwawa letu la Chinangali hapa Dodoma tayari kuna umwagiliaji wa matone katika zao la Mzabibu.

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Mabwawa ya kuvuna maji ya Mvua pamoja na mifereji ya umwagiliaji ili kupunguza athari za mvua katika Mkoa wa Kilimanjaro?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS L. MTEGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa mabwawa sita Wilayani Mbarali ili kuboresha kilimo cha mpunga?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika miradi yetu yote sita iliyoko Mbarali tumemaliza taratibu zote na miradi mingine wakandarasi tayari wako site. Miradi kama ya Utuo, Isenyera, Gonakuvagogoro, Helmanichosi yote yana mkandarasi na kazi inaendelea. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ya Awamu ya Sita imedhamiria kujenga miradi hiyo na kazi inaendelea.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Mabwawa ya kuvuna maji ya Mvua pamoja na mifereji ya umwagiliaji ili kupunguza athari za mvua katika Mkoa wa Kilimanjaro?

Supplementary Question 3

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kuna changamoto kubwa sana kwenye ukanda wa joto wa Mufundi kwenye zile kata Saba nadhani unazifahamu Mheshimiwa Naibu Waziri, Nyororo, Maduma, mbalamaziwa, Ihoanza, Itandula pamoja na Idunda;

Je, ni lini sasa Serikali watatuletea scheme za umwagiliaji ili wananchi wa pale waweze kulima kipindi chote?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika,napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja kati ya kazi kubwa ambayo tutaifanya katika mwaka wa fedha ujao ni kuhakikisha scheme zote za umwagiliaji tunazozijenga zinakuwa na chanzo cha maji ili wakulima waweze kulima mwaka mzima. Mheshimiwa Mbunge katika bajeti inayokuja maeneo uliyo yataja tutachimba mabwawa kwa ajili kuanza scheme za umwagiliaji ili wananchi wetu waweze kulima mwaka mzima.

Name

Aleksia Asia Kamguna

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Mabwawa ya kuvuna maji ya Mvua pamoja na mifereji ya umwagiliaji ili kupunguza athari za mvua katika Mkoa wa Kilimanjaro?

Supplementary Question 4

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Mkoa wa Morogoro kuna maeneo mengi yana maji ya kutosha;

Je ni lini sasa Serikali itajenga scheme ya umwagiliaji katika maeneo ya Mvomero na maeneo ya Mofu katika Halmashauri ya Mlimba?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Mkoa wa Morogoro una maeneo mengi yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji na tunayo miradi mingi ambayo inaendelea. Maeneo ambayo ameyataja nayachukulia kwa uzito mkubwa na hivyo nitaagiza wataalam wangu waende kuyaangalia, ili kama yanafaa basi tuyaingize katika mpango wetu ili kuhakikisha kwamba wakulima wanalima kupitia kilimo cha umwagiliaji.

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Mabwawa ya kuvuna maji ya Mvua pamoja na mifereji ya umwagiliaji ili kupunguza athari za mvua katika Mkoa wa Kilimanjaro?

Supplementary Question 5

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, kwa kuwa Serikali ilikuja kujenga miundo mbinu ya umwagiliaji kwenye bwawa kwenye Bonde la Bigombo liliko Ngara mwaka 2013 na kwa kuwa Serikali ilitelekeza bwawa hilo na miundombinu yake mwaka huo huo wa 2013;

Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuja kujenga lile bwawa na kulikamilisha?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimesikia kilio cha Mheshimiwa Mbunge juu ya mradi wa scheme ya Bigombo ambayo ameutaja. Namwelekeza Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na timu yake nzima kwenda kuliangalia bwawa hilo na scheme hiyo ili kujua changamoto iliyopo tuweze kuitatua. Kwa hiyo nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, timu yangu itaelekea huko kwenda kuangalia,
lengo letu ni kuhakikisha kwamba wananchi wetu wanafanya kilimo cha umwagiliaji.

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Mabwawa ya kuvuna maji ya Mvua pamoja na mifereji ya umwagiliaji ili kupunguza athari za mvua katika Mkoa wa Kilimanjaro?

Supplementary Question 6

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza;

Je, ni nini mpango au Mkakati wa Serikali kujenga scheme ya umwagiliaji katika ukanda ule wa delta kule kwetu Kibiti?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha tunayatumia mabonde yote makubwa nchini kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji. Tarehe 30 mwezi wa tatu mwaka 2023 mbele ya Mheshimiwa Rais, wakandarasi 22 walisaini mkataba wa mabonde yote ya kimkakati likiwemo bonde la Rufiji, Mto Ngono, Mto Manongawembele, Ziwa Victoria, Mto Luhuhu, Mto Songwe, Mto Ruvuma, Ifakara Idete na mpaka Litumbandio kwa Mheshimiwa Benaya Kapinga.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Mabwawa ya kuvuna maji ya Mvua pamoja na mifereji ya umwagiliaji ili kupunguza athari za mvua katika Mkoa wa Kilimanjaro?

Supplementary Question 7

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kunipa nafasi. Mradi wa umwagiliaji wa Arusha chini upo katika bajeti ya mwaka huu kwa ajili ya kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu lakini hadi sasa kazi hiyo haijafanywa. Je, ni lini kazi hiyo itafanyika?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama Mheshimiwa Mbunge alivyosema ipo miradi ambayo tuko hatua za mwisho za manunuzi ikiwemo mradi huo. Kwa hiyo nimwondoe hofu kwamba ilikuwa imeshapangwa na itatekelezwa kama ilivyopangwa, ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Mabwawa ya kuvuna maji ya Mvua pamoja na mifereji ya umwagiliaji ili kupunguza athari za mvua katika Mkoa wa Kilimanjaro?

Supplementary Question 8

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, Swali langu nilikuwa nataka kujua, Serikali itueleze kiujumla imejipangaje kuendeleza kilimo cha umwagiliaji kimkakati kitaifa katika mabonde yale ya kimkakati kitaifa yakiwemo na mabonde ya Namtumbo katika Bonde la Mwangaza, Liyuni, Likonde, Kitanda, Lusewa, Amani, Namahoka na Nambecha?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimetoka kusema hivi sasa, kwamba Serikali tunayo dhamira ya dhati kabisa kuhakikisha kwamba tunayatumia mabonde yote ya kimkakati katika kilimo cha umwagiliaji ili kuwawezesha wananchi wetu kulima mwaka mzima na zaidi ya mara mbili katika mwaka na maeneo ambayo ameyataja ni katika Mkoa wa Ruvuma.

Mheshimiwa Spika, eneo la Namtumbo pia tumeliweka katika mkakati wetu lakini kwa hivi sasa katika Mkoa wa Ruvuma tayari tunalo Bonde la Mto Luhuhu ambapo pale tuna zaidi ya hekta 3700; ambayo tumeanza kuyafanyia kazi, pamoja pia na bonde la Mto Ruvuma. Kwa hiyo sehemu ya Namtumbo ambao ameitaja Mheshimiwa Mbunge tutakwenda kuyapitia ili kuona, kama yanafaa tutayaingiza katika utaratibu wa kilimo cha umwagiliaji.

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Mabwawa ya kuvuna maji ya Mvua pamoja na mifereji ya umwagiliaji ili kupunguza athari za mvua katika Mkoa wa Kilimanjaro?

Supplementary Question 9

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi; nataka kujua ni lini scheme ya umwagiliaji itajengwa Makwale Wilayani Kyera?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, scheme ya Makwale Wilayani Kyera ni moja kati ya scheme muhimu sana kwa wakulima wa Wilaya ya Kyera. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, kwamba tarehe 25/4/2023 tunakwenda kusaini mkataba na mkandarasi na kazi itaanza mapema kwa ajili ya ujenzi wa scheme hiyo.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga Mabwawa ya kuvuna maji ya Mvua pamoja na mifereji ya umwagiliaji ili kupunguza athari za mvua katika Mkoa wa Kilimanjaro?

Supplementary Question 10

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsante, scheme ya umwagiliaji ya Mkoka ni moja ya scheme ambazo zimeharibiwa na mvua zilizokuwa zinaendela na hivyo kuleta kero kwa wakulima; Mheshimiwa Waziri unatusaidiaje kwa ghafla au kwa dharula?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika,napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nitaelekeza timu yangu ya wataalam kuangalia athari iliyojitokeza na tuweze kukarabati scheme hiyo ili wananchi waendelee na kilimo cha umwagiliaji.