Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 12 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 145 2023-04-24

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG’WASI D. KAMANI K.n.y. MHE. LATIFA K. JUWAKALI aliuliza: -

Je, upi mkakati wa Serikali wa kukuza ujuzi na stadi kwa vijana?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Latifah Khamis Juakali Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kukuza ujuzi na stadi za kazi kwa vijana, Serikali imeandaa Mkakati wa Taifa wa Kukuza Ujuzi wa miaka 10 (2016/2017 na 2025/2026) ambapo umelenga kuhakikisha nguvu kazi ya vijana inashiriki katika kujenga uchumi wa Taifa. Mkakati huu unatekelezwa kupitia program na mipango mbalimbali ya kukuza ujuzi na stadi kwa vijana inayotekelezwa na wadau mbalimbali wakiwemo Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Baadhi ya programu na mipango hiyo ni pamoja Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi inayotekelezwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu ambayo tangu kuanza kutekelezwa mwaka 2016/2017 imetoa mafunzo ya ujuzi na stadi za kazi kwa jumla ya vijana 118,415 na Mpango wa Mafunzo na Uwezeshaji wa Vijana kushiriki kilimo unaotekelezwa na kuratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu lakini kutekelezwa na Wizara ya Kilimo, ahsante.