Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG’WASI D. KAMANI K.n.y. MHE. LATIFA K. JUWAKALI aliuliza: - Je, upi mkakati wa Serikali wa kukuza ujuzi na stadi kwa vijana?

Supplementary Question 1

MHE. NG’WASI D. KAMANI: Mheshimiwa Naibu Spika,nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali; nina maswali mawili ya nyongeza.

i. Serikali inatumia mfumo gani kutathmini tija na matokeo ya programu hizo hasa ukizingatia kasi kubwa ya mabadiliko ya sayansi na teknolojia iliyopo sasa?

ii. Serikali ina makakati gani wa kuhakikisha kwamba Vijana wengi wananufaika na programu hizo ukizingatia uhitaji ni mkubwa kuliko nafasi zinazopatikana?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI, MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, ameuliza maswali mawili ya nyongeza; la kwanza ni kuhusu mfumo wa namna gani tunafanya tathmini kwa vijana hawa. Chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu ipo Idara ya Maendeleo ya Vijana. Chini ya mkurugenzi huyo kuna timu maalum ambayo inafanya tathmini ikiwa ni pamoja na kuweka mifumo na utaratibu wa kuweka kanzidata katika vyuo husika ambavyo tunawapitisha vijana hao kupata mafunzo. Kwa hiyo tunabaki na takwimu kwa ajili ya kuwawezesha pia baada ya mafunzo waweze kupata fursa za ajira lakini zaidi tunawapa pia hadi vifaa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika,kuhusu swali la pili nalo ameuliza kuhusu vijana, sikuweza kulipata vizuri nikuombe kwa ridhaa yako, niweze kulisikia vizuri.

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG’WASI D. KAMANI K.n.y. MHE. LATIFA K. JUWAKALI aliuliza: - Je, upi mkakati wa Serikali wa kukuza ujuzi na stadi kwa vijana?

Supplementary Question 2

MHE.NG’WASI D. KAMANI: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha vijana wengi zaidi wananufaika na programme hizo ukizingatia uhitaji ni mkubwa kuliko nafasi zinazopatikana?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya mikakati ambayo Wizara imeweka ni pamoja na huo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ya kuhakikisha vijana wengi wanaingia kwenye blue economy, kwa maana ya ufugaji wa samaki. Mkakati mwingine ni huu wa ukuzaji ujuzi ambapo tayari tumefundisha vijana zaidi ya 74,598, lakini pili upo mkakati mwingine huu ambao uko chini ya Wizara ya Kilimo unaoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu wa BBT ambapo tayari vijana 821, na Mheshimiwa Rais alizindua programme hiyo.

Meshimiwa Naibu Spika, tunao mkakati mwingine kupitia NACTVET pamoja na mafunzo ya TEHAMA ambayo tunaendelea nayo. Vilevile tuna Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa ambao unatutaka tuweze kuwafikia vijana zaidi ya 681,000 kwa kipindi hiki katika mpango huo wa miaka mitano. Tayari Serikali imeanza engagement na wadau wa maendeleo wakiwemo GIZ, International Labour Organisation pamoja na wadau wengine ni pamoja na Serikali yenyewe katika kuweka fedha kuhakikisha mafunzo haya tunayatoa kwa vijana walio wengi zaidi na kuwatafutia ajira ndani na nje ya nchi, ahsante.