Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 12 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 148 2023-04-24

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE: aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka magari ya kubebea wagonjwa katika Vituo vya Afya vya Mtwango na Mgololo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile, Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu na uhitaji wa magari ya kubebea wagonjwa katika vituo vya kutolea huduma za afya. Kwa kutambua mahitaji yaliyopo, Serikali katika mwaka wa fedha 2022/2023 imetenga shilingi bilioni 35.1 kwa ajili ya ununuzi wa magari 316 ya kubebea wagonjwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, taratibu za manunuzi zinaendelea na magari hayo yatagawiwa kwenye halmashauri zote 184 ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi ambayo itapewa magari 2 ya kubebea wagonjwa, ahsante.