Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE: aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka magari ya kubebea wagonjwa katika Vituo vya Afya vya Mtwango na Mgololo?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ya kuahidi kuleta magari mawili kwenye hivi vituo viwili cha Mtwango pamoja na cha Mgololo. Swali langu la nyongeza ni moja.

Je, kwa kuwa wananchi katika maeneo haya wameonesha jitihada kubwa za kuanza kujenga vituo hivyo vya afya, Serikali iko tayari kuleta fedha ili vikamilike mara moja kutokana na uhitaji mkubwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile, Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge amewasilisha hoja hizi za Vituo vya Afya vya Mtwango na Mgololo. Niwapongeze wananchi wa Jimbo la Mufindi Kusini kwa kuanza kujitolea nguvu zao. Nawahakikishia kwamba Serikali imeshaweka kwenye mpango wa kupeleka fedha ili kukamilisha vituo hivi vianze kutoa huduma kwa wananchi, ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE: aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka magari ya kubebea wagonjwa katika Vituo vya Afya vya Mtwango na Mgololo?

Supplementary Question 2

MHE ALLY M. KASINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Nanjilinji ambayo ina umbali wa zaidi ya kilomita 100 kutoka sehemu ya kutolea huduma ya afya kwa maana ya Hospitali ya Wilaya pale Kinyonga haina gari la wagonjwa.

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kupeleka gari la wagonjwa kwa ajili ya Kituo cha Afya Nanjirinji?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Kassinge, Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iliahidi kupeleka gari la wagonjwa katika Kituo cha Afya cha Nanjirinji na nimhakikishie kwamba kwenye magari ambayo tayari yameanza kununuliwa, tayari magari 117 yameingia kati ya 316 na kituo hiki kitapewa kipaumbele kupewa gari la wagonjwa, ahsante.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE: aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka magari ya kubebea wagonjwa katika Vituo vya Afya vya Mtwango na Mgololo?

Supplementary Question 3

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Katika Halmashauri yetu ya Wilaya ya Kilwa ina majimbo mawili; je, Serikali ina mpango gani wa kuleta ambulance zaidi ya moja ili kukidhi uhitaji katika Wilaya yetu ya Kilwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kusini, kama Ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunapeleka magari ya wagonjwa kwenye kila halmashauri, lakini ndani ya halmashauri kuna vipaumbele vya maeneo ambayo yana uhitaji mkubwa zaidi wa magari ya wagonjwa. Kwa hiyo, tunapeleka magari mawili katika Halmashauri ya Kilwa, lakini pia kukiwa na uhitaji na vigezo vya kutosha, basi tutaona namna ya kuepeleka gari nyingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE: aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka magari ya kubebea wagonjwa katika Vituo vya Afya vya Mtwango na Mgololo?

Supplementary Question 4

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Jimbo la Buchosa lina idadi ya watu wasiopungua 400,000 na vituo vya afya vinane, lakini lina gari la wagonjwa moja na watu wengi wanaishi visiwani. Je, Serikali iko tayari sasa kutamka kwamba Jimbo la Buchosa litapata magari ya wagonjwa katika miongoni mwa magari haya ya wagonjwa yanayotolewa na moja lipelekwe visiwani?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Buchosa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwamba katika magari 316 ya wagonjwa, Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa pia itapelekewa magari mawili ya wagonjwa, ahsante sana.