Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 12 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 150 2023-04-24

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: -

Je, ni kero zipi za Muungano zimetatuliwa na zipi zimebaki?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, hadi sasa Serikali za pande mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zimejadili na kuzipatia ufumbuzi jumla ya changamoto 22. Baadhi ya changamoto hizo ni: -

(i) Gharama za Kushusha Mizigo Bandari ya Dar es Salaam kwa Mizigo inayotoka Zanzibari;

(ii) Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia; na

(iii) Utaratibu wa Vikao vya Kamati ya Pamoja ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya Kushughulikia Masuala ya Muungano.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, changamoto zote zilizopatiwa ufumbuzi zimefafanuliwa kwa kina na zinapatikana katika tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais.

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja zilizobakia kutatuliwa ni nne ambazo ni: -

(i) Mapendekezo ya Tume ya pamoja ya Fedha;

(ii) Usajili wa Vyombo vya Moto;

(iii) Uingizaji wa Sukari katika Soko la Tanzania Bara; na

(iv) Mgawanyo wa Mapato yatokanayo na Hisa za SMZ zitakazokuwa katika Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki na faida ya Benki Kuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.