Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 12 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 151 2023-04-24

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka fedha Ludewa kwa ajili ya Miradi ya Ufugaji Samaki kwenye vizimba ndani ya Ziwa Nyasa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Zacharius Kamonga, Mbunge wa Ludewa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ufugaji wa samaki kwa vizimba ziwani unafanyika katika maeneo yaliyokidhi vigezo vya kisheria na kitaalam. Serikali kupitia Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) hufanya tathmini ya kimkakati ya mazingira (Strategic Environmental Assessment) ili kuhakikisha maeneo husika yanakidhi vigezo kabla ya kuanza uwekezaji. Tathmini hii imepangwa kufanyika kwa awamu katika Maziwa yetu yote na kwa mwaka 2021/2022 na 2022/2023 ilianza katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa Victoria.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka 2023/2024, Serikali imepanga kuendelea kufanya tathmini katika Ziwa Nyasa ikiwemo Ludewa ili kutambua maeneo yanayofaa kwa ufugaji samaki katika vizimba. Pia, Serikali itawezesha TAFIRI kufanya majaribio ya ufugaji samaki kwa kushirikiana na wananchi utakaojumuisha uzalishaji wa vifaranga vya samaki aina ya magege (Oreochromis karongae) na ufugaji wake kwa vizimba. Hatua hii inalenga kuwajengea uwezo wananchi wa ufugaji wa samaki pindi tathmini itakapokamilika. Vile vile, hatua hii itawawazesha wananchi wa Ludewa na Ziwa Nyasa kwa ujumla kunufaika na fursa za mikopo zilizopo kwa ajili ya kuwezesha ufugaji samaki kwa vizimba. Ahsante.