Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka fedha Ludewa kwa ajili ya Miradi ya Ufugaji Samaki kwenye vizimba ndani ya Ziwa Nyasa?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri na pia atupelekee shukrani nyingi Serikalini kwa kutuletea milioni 800 kwa ajili ya ujenzi wa Soko la Samaki pale Manda. Pamoja na Shukrani hizo naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; kule Ludewa wananchi wana ng’ombe kama 33,871 wa kienyeji na 687 wa kisasa ambao sio bora sana.

Je, Serikali ina mpango gani wa kutuletea madume bora kwa ajili ya kuboresha uzao wa ng’ombe kule Ludewa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ningependa kufahamu Serikali ina mkakati gani wa kurekebisha, Sheria Sera na Kanuni ili ziweze kusimamia Sekta ya Uvuvi ipasavyo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili nyongeza ya Mheshimiwa Kamonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, tunapokea shukrani na pili Program ya Uboreshaji wa Mifugo inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni program endelevu inayotumia njia ya madume bora na njia ya uhimilishaji. Yeye ameomba madume bora na katika mwaka huu wa fedha tunaoelekea 2023/2024, mkakati huu utaendelea na Ludewa tutaiweka kwenye eneo mojawapo la kunufaika na program hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, juu ya Sera, Sheria na Kanuni zetu tumekuwa tukifanya hivi na kila mara panapotokea hitaji, tutaendelea kuboresha Sheria na Kanuni zetu. Kwa hiyo kama Mheshimiwa Mbunge analo jambo mahususi tunamkaribisha kwa ajili ya kufanya maboresho hayo. Ahsante.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka fedha Ludewa kwa ajili ya Miradi ya Ufugaji Samaki kwenye vizimba ndani ya Ziwa Nyasa?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza swali la nyongeza. Serikali imewahi kwenda kutoa elimu ya ufugaji wa vizimba vya samaki kwa wananchi wanaozunguka Ziwa Basutu. Je, kwa kuwa imekwishakuwa ni muda mrefu ni lini Serikali itapeleka fedha ili wananchi hao waweze kunufaika na mafunzo hayo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia Halamga, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Manyara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tayari wananchi wa Basutu wamekwishapata elimu naomba nimuahidi kuwa Serikali inalichukua jambo hili na kwenyewe tutakwenda kufanya tathimini ya kimazingira ili waweze kunufaika na program hii na kujiongezea kipato na kutengeneza ajira. Ahsante sana.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka fedha Ludewa kwa ajili ya Miradi ya Ufugaji Samaki kwenye vizimba ndani ya Ziwa Nyasa?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. FAUSTINE NDUGULILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika majibu ya Mheshimiwa Waziri ameeleza kwamba kuna nguvu kubwa sana imepelekwa katika ukanda wa Maziwa katika suala zima la ufugaji wa samaki kwa vizimba. Je, nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha kwamba na Ukanda wa Pwani ikiwa ni pamoja na Kigamboni zinanufaika na uvuvi wa samaki kwa njia ya vizimba?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulile Mbunge wa Kigamboni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka huu wa 2022/2023 upande wa Mikoa ya Pwani kwenye programu hii ya ufugaji wa samaki tulipeleka pesa zaidi upande wa ukulima wa mwani Takribani Bilioni 2.1zimenufaisha wakulima wa mwani kutoka Tanga kule Moha mpaka Mtwara kule Msimbati, sasa katika mwaka wa 2023/2024 kupitia programu maalum ya blue economy tunatarajia kupeleka tena nguvu kwa maana ya uwezeshaji, kwa lengo la mwani vilevile unenepeshaji wa Kaa na ufugaji wa Majongoo Bahari. Kwa hivyo, wakulima na wavuvi wa ukanda wa Pwani wakiwemo wa Kigamboni na wenyewe makundi ya vijana na akina mama yatapata kunufaika na programu hii. Ahsante.