Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 12 Energy and Minerals Wizara ya Madini 152 2023-04-24

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: -

Je, ni lini Wananchi wa Kitongoji cha Nyamichele watalipwa fidia kutokana na madhila waliyoyapata kutoka Mgodi wa Barrick?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mgodi wa Barrick North Mara kwa sasa hauhitaji eneo la Kitongoji cha Nyamichele kama wananchi walivyokuwa wametarajia hapo kabla.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na Mgodi wa North Mara kutohitaji eneo hilo, kuna utaratibu ambao unaandaliwa na mgodi huo wa kutoa kifuta jasho kwa wananchi waliopata madhila kutoka kwa mgodi huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)