Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 12 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 156 2023-04-24

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO K.n.y. MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza: -

Je, nini mkakati gani wa kumaliza changamoto za ukosefu wa nyumba za askari, magari na ufinyu wa ofisi katika Kituo cha Polisi Mlandizi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Polisi Mlandizi kilichopo Mkoa wa Pwani, kina gari moja PT 4336 Ashok Leyland ambalo linafanya kazi. Kituo hicho kinatekeleza mradi wa ujenzi wa nyumba mbili za kuishi familia Sita za Askari. Ujenzi wa nyumba hizo ambao umegharimu Shilingi Milioni 106.92 umechangiwa na nguvu za wananchi na wadau. Jengo moja lipo kwenye hatua ya kumalizia na lingine liko kwenye hatua ya msingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kumalizia ujenzi wa nyumba zote mbili kiasi cha shilingi milioni 147.054 kinahitajika. Kuhusu mahitaji ya ofisi, tathmini kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Upelelezi, uchunguzi wa kisayansi na intelijensia ya jinai umefanyika na kubaini kuwa kiasi cha fedha shilingi 82,000,000 kinahitajika.

Mheshimiwa Naibu Spika, fedha kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa nyumba za nyumba za askari, pamoja na ofisi zitaombwa kwenye Mfuko wa Tuzo na Tozo katika mwaka wa fedha 2023/2024. Nashukuru.