Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO K.n.y. MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza: - Je, nini mkakati gani wa kumaliza changamoto za ukosefu wa nyumba za askari, magari na ufinyu wa ofisi katika Kituo cha Polisi Mlandizi?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Swali la kwanza, kwa kuwa gari analolizungumza Mheshimiwa Naibu Waziri ni gari aina ya lori na kituo kile kina shughuli nyingi za kipolisi kwa sababu eneo la Mji wa Mlandizi limejengeka. Je, Serikali haioni iko haja sasa ya kuwapelekea gari dogo litakaloendana sawa na kasi ya kukabiliana na uhalifu katika Mji ule?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili jengo la Kituo cha Polisi Mlandizi linatumika kwa ajili ya OCS pamoja na OCD, sasa kwa kuwa jengo hili ni dogo hawaoni sasa ni muda muafaka wa kutafuta eneo lingine kuzitofautisha ofisi hizi? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwakambo Michael, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mosi, tunatambua kwamba lori kwa kweli lina changamoto kwenye ufuatiliaji wa doria hasa kwenye vichochoro na njia kama hizo, lakini kwa shughuli nyingi za kiuchumi zinazoendelea pale Mlandizi wanayo kweli haki ya kupata gari ndogo. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mwakambo pamoja na Wabunge wote kwamba Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Jeshi la Polisi, karibuni itapata magari kwa ajili ya kuwezesha ofisi zote za ma OCD kupata gari ndogo kuwezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu jengo hili, tumeeleza ofisi zitakazoongezeka kama kwenye jibu langu la msingi tulivyosema lakini kutokana na hoja kwamba eneo ni dogo, namwomba Mkurugenzi, kwa maana ya Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, kutafuta eneo, na pale litakapokuwa limepatikana, sisi always tutakuwa tayari kushirikiana na Halmashauri hiyo kuimarisha majengo yanayotakiwa kwenye kituo kile, nashukuru.