Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 12 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 155 2023-04-24

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: -

Je, ni lini kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Mabokweni – Maramba – Daluni – Bombomtoni – Magoma – Korogwe utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dustan Luka Kitandula, Mbunge wa Mkinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania imeanza na inaendelea na kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami kwa Barabara ya Mabokweni – Bombomtoni – Mashewa – Magoma – Kwamndolwa hadi Old Korogwe urefu wa kilometa 127.69. Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ilianza mwezi Agosti, 2022 na inatarajiwa kukamilika mwezi Septemba, 2023, ahsante.