Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Mabokweni – Maramba – Daluni – Bombomtoni – Magoma – Korogwe utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, nyaraka za kiofisi tulizonazo kutoka Serikalini zilionesha kwamba katika barabara hii, usananifu na upembuzi yakinifu ungekamilika mwezi wa Sita lakini sasa tunaambiwa ni mwezi wa Tisa: Je, Waziri anaweza kuniambia mpaka sasa kazi iliyofanyika, imefanyika kwa kiwango cha asilimia ngapi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kutokana na umuhimu wa barabara hii kiusalama na kiuchumi, Wizara ipo tayari kutenga fedha ili ujenzi uweze kufanyika kwenye lots ambazo kazi imeshakamilika? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Dunstan Luka Kitandula, Mbunge wa Mkinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu asilimia ambayo imefikiwa, naomba baada ya kikao hiki niweze kupata taarifa kamili kwa sasa tuko asilimia ngapi? Hata hivyo nataka tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba pengine kitu muhimu hapa ni lini tutakamilisha hii kazi ambayo kwenye jibu langu la msingi nimesema kazi hii ya usanifu itakamilika mwezi Septemba. Kwa maana ya takwimu, asilimu naomba nitamjulisha Mheshimiwa Mbunge mara baada ya kutoka hapa kupata taarifa kamili.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunatambua kwamba barabara hii ni muhimu sana kiusalama na kiuchumi na ndiyo maana tumeamua kuifanyia usanifu wa kina ili barabara hii iweze kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)