Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 12 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 158 2023-04-24

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza: -

Je, ni vijana wangapi wa Tanzania wamepata nafasi za masomo nje ya Nchi kwa mwaka 2015-2020 na wangapi wanatoka Zanzibar?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU K.n.y. WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nafasi za ufadhili wa masomo unaotolewa na mashirika au nchi rafiki zinazopitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, huratibiwa kwa ushirikiano baina ya pande mbili za Muungano. Idara za elimu ya juu zina jukumu la kubaini sifa za waombaji na kupendekeza wanufaika wa ufadhili kwa kuzingatia vigezo bila kujali mwombaji anatoka upande upi wa Muungano. Aidha, zipo baadhi ya nafasi za ufadhili wa masomo ambazo huratibiwa moja kwa moja na nchi au shirika linalotoa ufadhili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka 2015 - 2020, Wizara ya Elimu, Sayani na Teknolojia kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar iliratibu ufadhili wa masomo katika nchi za Uingereza, Hangaria, China, Morocco, Misri, Algeria, Urusi, Ujerumani, Msumbiji, Thailand, Mauritius, Iran na Indonesia. Watanzania walionufaika na ufadhili huo ni 873 ambapo kati yao wanaume ni 587 na wanawake 286.