Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza: - Je, ni vijana wangapi wa Tanzania wamepata nafasi za masomo nje ya Nchi kwa mwaka 2015-2020 na wangapi wanatoka Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante; kwanza sina budi kuishukuru Serikali kwa jibu lake zuri lenye mafanikio kwa wananchi. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali inafanya juhudi kubwa kusomesha vijana wake ili kufaidika nao; je, baada ya kuhitimu masomo hayo, Serikali inafaidika kitu gani wakati vijana hao wanabakia vijiweni? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili: Kwa kuwa Serikali haina ajira kwa watu wote, na vijana hawa tayari wamesoma; je, Serikali inawatengenezea mazingira gani vijana hawa ili nao waweze kuishi maisha bora? Ahsante. (Makofi)

Name

Prof. Joyce Lazaro Ndalichako

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge pamoja na Bunge lako kwamba, Serikali inapata manufaa makubwa sana kwa kupeleka vijana kusoma nje ya nchi, kwa sababu licha ya ujuzi na maarifa ambayo wanapata, lakini vijana hao pia wanapata uzoefu kutoka nchi nyingine; kutoka nchi ambayo wanafunzi wanasoma lakini pia na nchi ambazo zinakuwa zimepeleka wanafunzi katika chuo husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili kwamba Serikali haina ajira na je, inatengeneza mazingira yapi kwa vijana hawa wanaotoka nje ya nchi: Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imeendelea kuwa inatoa ajira kupitia ajira zinazotangazwa na Sekretarieti ya Ajira na pia kupitia sekta binafsi ambayo inakua kwa kasi kubwa. Vile vile, Serikali imeendelea kutengeneza mazingira kwa kuwapa nafasi za kupata mafunzo ya uzoefu kazini wakati wakiwa wanasubiri kupata ajira.