Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 12 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 159 2023-04-24

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuunganisha mifumo ya utoaji leseni katika Sekta ya Utalii ili kurahisisha upatikanaji wa leseni?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tayari imeshaunganisha mfumo wa utoaji wa leseni katika sekta ya utalii kupitia mfumo wa kieletroniki wa MNRT – Portal. Hatua hiyo imeongeza tija katika utoaji huduma ikiwemo kurahisisha mchakato wa utoaji wa leseni za biashara za utalii na hivyo kupunguza gharama, muda na kuongeza wigo wa ushiriki wa wananchi na wawekezaji mbalimbali katika biashara hizo.