Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuunganisha mifumo ya utoaji leseni katika Sekta ya Utalii ili kurahisisha upatikanaji wa leseni?

Supplementary Question 1

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza. Je, ni lini mifumo ya malipo ya TANAPA, TAWA, Ngorongoro pamoja na ile ya Wizara itaunganishwa na kuwa mfumo mmoja wa malipo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni lini Serikali itaruhusu uhai wa leseni za TALA uwe kwa mwaka ambao leseni imekatwa tofauti na sasa hivi ambavyo leseni inakuwa ni kalenda ya mwaka?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mifumo ya malipo katika taasisi zetu tayari imeshaanza kutumika. Baadhi ya taasisi kama Ngorongoro na TANAPA utekelezaji wake unaendelea, lakini baadi ya taasisi tayari tulishaunganisha. Kwenye upande wa leseni; sasa hivi leseni inatoka kwa mfumo mmoja tu ambapo imeunganishwa mifumo yote. Kwa hiyo, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba kwenye suala la leseni wadau wote wanafaidika na mfumo huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye suala hili lingine la TALA, tumeshaanza kupokea maoni kutoka kwa wadau mbalimbali hususan wadau wa masuala ya utalii na tunaangalia tupitie kanuni upya tuone kama zitaleta tija katika marekebisho ya utoaji wa leseni. Nawakumbusha tu wadau hawa kwamba Serikali ina calenda year ambapo ndiyo huwa inakusanya mapato yake na imejiwekea mipango yake. Kwa hiyo, kama tutaona kuna haja ya kurekebisha kanuni hizi, basi tutawashirikisha kwa kuchukua maoni yao, lakini kwa kuangalia pia Serikali katika ukusanyaji wa mapato, ahsante. (Makofi)