Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 14 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 175 2023-04-27

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza: -

Je, lini Mfuko wa Taifa wa Watu wenye Ulemavu utaanza kufanya kazi?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Ikupa Alex, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mfuko wa Taifa wa Watu Wenye Ulemavu umeanzishwa kwa mujibu wa Kifungu cha 57 cha Sheria ya Watu Wenye Ulemavu Na. 9 ya mwaka 2010. Katika kutimiza azma ya Serikali ya uanzishwaji wa Mfuko huu, hatua mbalimbali zimeshachukuliwa na Serikali ikiwemo uandaaji wa Mwongozo wa Usimamizi, Uratibu na Uendeshaji wa Mfuko husika pamoja na kufunguliwa kwa akaunti ya mfuko.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kukamilika kwa hatua zote muhimu za mfuko kuanza kutekeleza majukumu yake, mfuko huu haujaanza kutoa huduma kutokana na maelekezo ya kuunganisha mifuko yote ya uwezeshaji wananchi kiuchumi yaliyotolewa mwaka 2020. Zoezi hili liliambatana na tathmini ya ufanisi wa utendaji wa mifuko. Aidha, tathimini hii itakapokamilika, wadau wote wataarifiwa juu ya uanzishwaji wa mifuko hiyo ukiwemo Mfuko huu wa Taifa wa Watu wenye Ulemavu, ahsante.