Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza: - Je, lini Mfuko wa Taifa wa Watu wenye Ulemavu utaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa hatua zote za uanzishwaji wa mfuko huu zilikwisha kamilika, ninaomba kufahamu tathmini iliyoelezwa kwenye jibu la msingi itakamilika lini.

Mheshimiwa Spika, kutokana na umuhimu wa mfuko huu kwa watu wenye ulemavu, Serikali inaonaje ikauacha mfuko huu ujitegemee kuliko kuuunganisha na mifuko mingine? Ahsante.

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa
Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stella Ikupa Alex, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tathmini inayofanyika kwa sasa lilikuwa ni suala tu la kibajeti na kwa mwaka huu wa fedha tunakwenda kulikamilisha hilo kwa sababu tayari mipango yote imekwisha kukamilika.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili la mfuko kutokuunganishwa na mifuko mingine. Ni kweli lakini pamoja na hilo tunatambua kundi hili ni muhimu sana na ni kundi ambalo ni maalum. Kwa umaalum wake tumekwisha kuona katika eneo la tathmini ni pamoja na kutambua kwanza vyanzo vya mapato na sera na sheria ambazo zitaongoza mfuko husika.

Mheshimiwa Spika, tatu, ni usimamizi wa fedha hizo, na nne, ni jinsi gani ambavyo fedha hizi zinazopatikana, zipo zitakazopatikana kutokana na ruzuku ya Serikali, lakini kwa sababu ya umaalum wake, zipo fedha ambazo zitatokana na wadau ndiko huko kunakopeleka umuhimu wa baadhi ya mifuko kusimama yenyewe kwa sababu msingi wa mfuko huu unaanzishwa na Sheria Na. 9 ya mwaka 2010 ambayo inataka uwepo wa mfuko huu. Kwa hiyo, kuna mifuko ambayo baada ya tathmini haitakuwa imeungwanishwa pamoja.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya tathmini tutakuwa tumepata picha kamili ya namna ya kuongoza mfuko huu ili uweze kuleta tija na faida zaidi kwa ndugu zetu watu wenye ulemavu, ahsante.

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza: - Je, lini Mfuko wa Taifa wa Watu wenye Ulemavu utaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, kwa kuwa watu wenye ulemavu wameonekana mara nyingi wakiwa wanaombaomba na wakati mwingine kutumiwa kama chambo katika kuomba; je, ni mkakati upi wa Serikali katika kuwasaidia watu hawa kujikwamua kiuchumi?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa
Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Edwin Malleko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu namna ya kuwasaidia watu wenye ulemavu kutokana na suala la kuwa ombaomba. Moja ya mikakati ya Serikali ni kutoa elimu; kumekuwa na changamoto sana ya kubadilisha mindsets za watu wetu. Na slogan ya Serikali ambayo inatumika hapa ni disability is not inability; kwa hiyo tumekuwa tukitoa elimu. Sambamba na hilo, Serikali imefungua vyuo vya watu wenye ulemavu ili kuwawezesha waweze kupata ujuzi wa ufundi stadi.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, tumekwenda pia kwenye hatua nyingine ya kuweza kutoa mikopo kupitia halmashauri, asilimia mbili, kuwawezesha watu wenye ulemavu. Sambamba na hilo pia tumekwenda katika hatua nyingine ya kuhakikisha kwamba tunawasaidia watu wenye ulemavu katika kutengeneza miongozo mbalimbali ukiwemo huu wa kuweza kuwa na mfuko maalum pamoja na kuwawezesha na kuwaweka kwenye vyama ambavyo vitawasaidia kuweza ku-raise agenda zao na kuweza kusaidiwa na Serikali kwa ukaribu na kwa umoja zaidi.

Mheshimiwa Spika, kwenye eneo hilo la kuendelea kuwa na suala la ombaomba, tayari tumeshaweka mikakati mbalimbali ikiwemo kuweza kuongeza fedha katika mifuko ya watu wenye ulemavu ili waweze kupata elimu ya ujasiriamali na kujikwamua zaidi.

Mheshimiwa Spika, upande wa elimu, tayari tuna inclusive education ambapo kwa wale wenye uwezo wa kwenda shule Serikali imekuwa ikiwachukua. Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wetu, amekwisha kutoa zaidi ya bilioni tatu kwa ajili ya kurekebisha vyuo vya watu wenye ulemavu na kutoa huduma za utengemavu, ahsante.

Name

Khadija Shaaban Taya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza: - Je, lini Mfuko wa Taifa wa Watu wenye Ulemavu utaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 3

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika nashukuru sana, ningeomba kujua kwenye hii Wizara ilitolewa milioni 60 kwa ajili mafuta ya watu wenye uarubino. Nataka nifahamu ni lini sasa yale mafuta yataanza kusambaa Tanzania nzima, kwa sababu nina amini kuna Wabunge hapa wananiuliza kila siku wanahitaji haya mafuta? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE.PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa
Spika, hili ni la kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa sababu aliona umuhimu huo. Tulikuwa tunapata mafuta kutoka nje ya nchi sasa yanatengenezwa pale KCMC, na gharama zinalipwa na Mheshimiwa Rais wa Serikali ya Awamu ya sita. Suala la usambazaji na ufikaji wa mafuta ni suala la uratibu tu ambalo nitaomba Mheshimiwa Mbunge niwasiliane naye kama kuna changamoto sehemu za wao kuweza kuyapata; lakini pia tutaweka utaratibu wazi wa kuweza kuona ni namna gani kila eneo wataweza kuyapata mafuta haya muhimu kwa ajili ya watu wetu wenye ulemavu, ahsante sana.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza: - Je, lini Mfuko wa Taifa wa Watu wenye Ulemavu utaanza kufanya kazi?

Supplementary Question 4

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika ahsante sana, kwa kuwa matibabu ya watu wenye ulemavu ni ya ghali sana kwa namna ya kuwapeleka hospitali lakini na hata matibabu yenyewe.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka ruzuku ya bima ya afya kwa ajili ya watu wenye ulemavu ili kuwapunguzia adha wazazi? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa
Spika, ahsante, moja ya jitihada za Serikali ni pamoja na kuandaa mwongozo huo wa mwaka 2020 ambao umekamilika katika kuona na kuratibu masuala ya changamoto, kwanza kutambua changamoto za watu wenye ulemavu lakini pili kuona namna gani tunaweza kuwahudumia zaidi. Kwa hiyo kuwepo kwa mfuko wa watu wenye ulemavu utatatua changamoto nyingi sana ambazo zitasaidia sana kuona namna gani tunaenda kutatuta changamoto hii.

Mheshimiwa Spika, kwenye suala la bima, kwa kuwa tuko kwenye utaratibu sasa wa kupata universal health care, mfuko wa bima ya afya kwa wote tutaona pia umaalum wake kwa sababu kundi hili ni muhimu kuweza kuliangalia kwa umaalum wake na kulifanya hilo. Kwa hiyo niseme tu nimepokea ushauri wa Mheshimiwa Mbunge na kwamba tutaufanyia kazi, ahsante sana.