Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 14 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 177 2023-04-27

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itahuisha mpango wa upanuzi wa Manispaa ya Moshi kutoka kilometa 58 hadi 146 pamoja na kuwa Jiji?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Priscus Jacob Tarimo Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI tarehe 25 novemba, 2015 ilipokea ombi la uendelezaji wa Manispaa ya Moshi kuwa Jiji kwa kuongeza ukubwa wa mipaka ya kiutawala kutoka kilomita za mraba 58 hadi kilomita za mraba 142 kwa kuongeza vijiji kutoka Halmashauri za Wilaya za Moshi na Hai.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Mwongozo wa Uanzishaji wa Maeneo ya Utawala wa mwaka 2014, kigezo cha ukubwa wa kuanzisha halmashauri ya jiji ni kilometa za mraba 1,000 na Halmashauri ya Wilaya ni kilometa za mraba 5,000.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mamlaka nyingi zilizoanzishwa bado zinaupungufu wa miundombinu mbalimbali yakiwemo majengo ya utawala na huduma za kijamii, kwa sasa Serikali imeweka kipaumbele katika uboreshaji wa miundombinu katika maeneo ya utawala yaliyopo.