Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itahuisha mpango wa upanuzi wa Manispaa ya Moshi kutoka kilometa 58 hadi 146 pamoja na kuwa Jiji?

Supplementary Question 1

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, kwa kuwa hitaji letu ni uhalisia kuliko nadharia, kutokana na uhalisia kwamba hata eneo la dampo sasa tumenunua Moshi Vijijini; na moja ya changamoto ni kwamba barabara inayoelekea kwenye dampo hatuwezi kuikarabai sisi kwa sababu haiwezi kuingia kwenye bajeti ikafanye kazi Moshi Vijijini. Na Moshi Vijijini pia haiko kwenye vipaumbele vyao kwa hiyo inatusababisha sisi tuna operate kwa gharama kubwa sana. Lakini pia inasababisha kwa mfano hospitali ya halmashauri inayojengwa Moshi Mjini inabidi ijengwe kwa ghorofa jambo ambalo ni karibu mara mbili ya gharama za kutengeneza maeneo mengine.

Je, tukiachana na Suala la Jiji ni lini mtakubali tupanue kuendana na GN namba 219 ya tarehe 15, July 2016 ikiwa ni pamoja na kupata maeneo ya makaburi ambayo hatuna?

Swali la pili; yapo maeneo kwenye kata, kwa mfano kata ya Shirimatunda, eneo la Boniti ambalo lilikuwa la viwanda lakini sasa hivi limesharasimishwa kuwa makazi lakini haliwezi kuendelea ili watu wapate hati zao kwa sababu ya kusubiri mchakato huo.

Je, hamuoni kwamba kuna uwezekano wa kutoa upendelea kwa Moshi Mjini kwanza?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa
Spika, nikienda kwenye swali lake la kwanza la Mheshimiwa Tarimo la uhitaji huu ni uhalisia; Serikali inatambua umuhimu wa kutanua mipaka ya Halmashauri ya Manispaa ya Moshi. Lakini kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, kwamba kwa sasa kipaumbele kikubwa ni kuhakikisha tunaimarisha yale maeneo ambayo ni mapya na halmashauri ambazo ni mpya. Ni muda si mrefu halmashauri nyingi zilihamia katika maeneo yao ya utawala, na kwa sasa Serikali hii ya Awamu ya Sita imeweka kipumbele kuhakikisha majengo ya utawala,kuhakikisha huduma za hospitali za Wilaya, kuhakikisha mashule na kadhalika yanajengwa, na hivyo baada ya haya kukamilika Serikali itaanza kutenga bajeti kuhakikisha maeneo mapya ya kiutawala yanatekelezwa.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili, niseme tu kuwa Serikali inalichukua hili ambalo Mheshimiwa Mbunge amelizungumza la Halmashauri ya Manispaa ya Moshi kupewa upendeleo maalumu kwa sababu tayari GN ilikuwepo. Pale ambapo tutamaliza ukamilishaji wa ujenzi wa miundo mbinu katika halmashauri mpya basi Moshi Mjini Manispaa nayo itapewa kipaumbele.