Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 17 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 213 2023-05-03

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza: -

Je, lini Serikali itaipatia fedha Halmashauri ya Manispaa ya Lindi ili iweze kutekeleza mradi wa kimkakati wa ujenzi wa Soko Kuu?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah, Mbunge wa Jimbo la Lindi Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi ni miongoni mwa miji 45 ambayo imepewa kipaumbele cha kupata ufadhili wa Mradi wa Uboreshaji Miundombinu ya Miji, Manispaa na Majiji ambapo ujenzi wa soko ni miongoni mwa miundombinu itakayotekelezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha upimaji eneo la ujenzi wa soko na kupata hati yenye ukubwa wa mita za mraba 5,845 pamoja na cheti cha Hati ya Tathmini ya Athari kwa Mazingira (EIA) kutoka NEMC kama sehemu ya lazima katika kuanza kwa mradi huu katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi.