Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza: - Je, lini Serikali itaipatia fedha Halmashauri ya Manispaa ya Lindi ili iweze kutekeleza mradi wa kimkakati wa ujenzi wa Soko Kuu?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza niishukuru Serikali kwa majibu hayo yenye kuleta matumaini. Pamoja na kwamba wamechukua hatua mbalimbali za upimaji wa eneo na kuchukua tathmini ya hati ya mazingira, ninaomba niulize swali moja la nyongeza: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Soko la Lindi Manispaa limejengwa mwaka 1950, kwa hiyo ni soko ambalo tumerithi kutoka kwa wakoloni, ni la muda mrefu tangu Lindi ikiwa eneo dogo na sasa hivi Lindi Manispaa ina kata 31 na makusanyo ya manispaa ni shilingi bilioni tatu kwa mwaka. Makusanyo ni madogo lakini tunatoa huduma katika kata 31.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lini Serikali itaona umuhimu mkubwa wa kutupatia fedha katika kuhakikisha kwamba tunakwenda kutekeleza mradi huu wa kimkakati wa ujenzi wa soko? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua shauku ya Mheshimiwa Mbunge juu ya soko hili, na amekuwa akilipambania tangu akiwa Mbunge wa Viti Maalum na mpaka sasa ni Mbunge wa Jimbo. Na ukweli ni kwamba Manispaa ya Lindi ipo katika Tier II katika miradi ambayo inaanza kutekelezwa katika Mwaka wa Fedha 2023/24, kwa hiyo nimuondoe shaka tu na wananchi wake kwamba utekelezaji wao utafanyika kama ambavyo watu wa Tier I sasa hivi wako katika hatua za mwisho, ahsante sana.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza: - Je, lini Serikali itaipatia fedha Halmashauri ya Manispaa ya Lindi ili iweze kutekeleza mradi wa kimkakati wa ujenzi wa Soko Kuu?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Liwale kwenye bajeti ya 2018-2020 tulitengewa fedha kwa ajili ya kujenga stendi ya kisasa kama mradi wa kimkakati, lakini fedha zile zilirudishwa kutokana na sababu zisizojulikana. Je, ni lini Serikali itatuletea fedha hizo tena ili mradi ule wa kimkakati uweze kukamilika kwa wakati?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Mohamedi Kuchauka, Mbunge wa Jimbo la Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri Bunge lako lilipitisha hapa sheria ya kuhakikisha kwamba fedha zote ambazo zimeelekezwa katika miradi na kuvuka mwaka wa fedha ziendelee kubaki ili zitekeleze miradi ambayo imekusudiwa. Na jambo hili alilozungumza Mheshimiwa Mbunge maana yake sasa Ofisi ya Rais, TAMISEMI italifanyia kazi kulipitia ili ione namna bora ya kuhakikisha fedha zile zinarudi na kufanya kazi ambayo imekusudiwa, ahsante sana.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza: - Je, lini Serikali itaipatia fedha Halmashauri ya Manispaa ya Lindi ili iweze kutekeleza mradi wa kimkakati wa ujenzi wa Soko Kuu?

Supplementary Question 3

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa Soko Kuu la Bukoba Mjini ni chakavu na dogo kwa matumizi ya sasa, je, lini Mradi wa TACTIC utaanza ili soko hilo lijengwe?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oliver Daniel Semuguruka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba Manispaa ya Bukoba iko katika awamu ya pili ya utekelezaji wa Mradi wa TACTIC (Tier II). Kwa hiyo nimwondoe hofu, kama ambavyo Mbunge wa Jimbo, Mheshimiwa Stephen Byabato analifuatilia na jambo hili linakwenda kutekelezeka. Ahsante.

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza: - Je, lini Serikali itaipatia fedha Halmashauri ya Manispaa ya Lindi ili iweze kutekeleza mradi wa kimkakati wa ujenzi wa Soko Kuu?

Supplementary Question 4

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ziara ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwenye Jimbo la Ukonga tarehe 23, Februari, alitoa maelekezo ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuanza mchakato wa ujenzi wa soko kwenye Kata ya Gongo la Mboto, soko ambalo litatumiwa na wafanyabiashara ambao kwa sasa wanafanya biashara barabarani na kutumiwa na zaidi ya kata tano. Je, Serikali imefikia wapi kwenye utekelezaji wa agizo hilo la Mheshimiwa Waziri? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jerry William Silaa, Mbunge wa Jimbo la Ukonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, maelekezo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI ambayo aliyatoa ni maelekezo ambayo Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala alishaelekezwa kuyatekeleza. Kwa hiyo, ninarudia tu kumwelekeza mkurugenzi wa manispaa kutekeleza ahadi ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ahsante.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza: - Je, lini Serikali itaipatia fedha Halmashauri ya Manispaa ya Lindi ili iweze kutekeleza mradi wa kimkakati wa ujenzi wa Soko Kuu?

Supplementary Question 5

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa kwa muda mrefu nimekuwa nikifwatilia juu ya ujenzi wa soko la mazao pale Vwawa;

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba lile soko linajengwa kama ambavyo imekuwa ikiahidi kwa muda mrefu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Japhet Ngailonga Hasunga, Mbunge wa Jimbo la Vwawa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati nzuri Mheshimiwa Hasunga tunatokea katika mkoa mmoja na anatambua kabisa Soko la Vwawa liko katika Mradi wa TACTIC Tier III kwa hiyo, utekelezaji wa mradi utakapoanza ambapo mimi na yeye tuko katika kundi moja, maana yake na yeye atapatiwa hiyo huduma. Ahsante sana.