Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 17 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 218 2023-05-03

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: -

Je, Serikali imetoa mwongozo gani kuhusiana na kiwango cha ubora wa taa zinazowekwa barabarani?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rehema Juma Migilla, Mbunge wa Ulyankulu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali haijatoa mwongozo rasmi kuhusiana na ubora wa taa zinazowekwa barabarani. Kwa sasa, Wizara imekasimisha shughuli za usimikaji wa mifumo ya umeme ikiwemo taa za kuongozea vyombo vya moto (traffic lights) na taa za usalama barabarani (street lights) kwa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) ambapo hutoa msawazo (specifications) wa taa kwa Taasisi nunuzi unaoendana na mazingira na teknolojia ya wakati husika kwa viwango vya kimataifa.