Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 17 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 219 2023-05-03

Name

Omar Ali Omar

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Wete

Primary Question

MHE. OMAR ALI OMAR aliuiliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka magari kwa jeshi la polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omar Ali Omar, Mbunge wa Wete, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kulipatia Jeshi la Polisi magari kama nyenzo ya kutendea kazi. mwaka 2022, Mkoa wa Kaskazini Pemba ulipatiwa magari matatu (3) yaliyonunuliwa na Serikali ili kupunguza uhaba wa magari katika mkoa huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Bajeti yake ya mwaka wa fedha 2022/2023, imetoa fedha kiasi cha Shilingi Bilioni 15 kwa Jeshi la Polisi kwa ajili ya kununulia magari na pikipiki. Pindi magari na pikipiki yatakapopokelewa yatagawiwa kwenye mikoa na wilaya zenye uhitaji mkubwa ikiwemo Mkoa wa Kaskazini Pemba, nashukuru.