Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Ali Omar

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Wete

Primary Question

MHE. OMAR ALI OMAR aliuiliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka magari kwa jeshi la polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ALI OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa taarifa nilizokuwa nazo kwamba magari ya polisi yaliyoko Mkoa wa Kaskazini Pemba ni mawili tu. Je, hili gari moja limekwenda sehemu gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; Jeshi La Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba lina magari machakavu mengi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuyatengeneza magari haya au kuyapiga mnada?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Omar kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa alizonazo yeye ni magari mawili, lakini taarifa nilizopewa na IGP ni magari matatu. Tutafuta hilo la tatu liko wapi, kama limepelekwa mahali fulani tutahakikisha linapelekwa Pemba ili magari matatu yaweze kutimia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uchakavu wa magari, tutafanya tathmini kama kawaida ilivyo kwa mali za Serikali, magari yaliyochoka yanafanyiwa tathmini, yanayoweza kufanyiwa ukarabati au matengenezo yakarejea barabarani yanafanyika, yale yanayoshindikana huuzwa kwa utaratibu unaosimamiwa na Wizara ya Fedha. Kwa hiyo, tutafanya tathmini ya haraka ili yale yaliyo machakavu kabisa tuyaondoe kwenye daftari kwa kuyauza na yale yanayoweza kutengenezeka yafanyiwe matengenezo, yasaidie usafiri wa vijana wetu, nashukuru.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. OMAR ALI OMAR aliuiliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka magari kwa jeshi la polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Wilaya ya Kahama ina mwingiliano mkubwa sana wa raia wa kigeni lakini Ofisi ya Immigration katika Wilaya ya Kahama haina gari kabisa na haina kabisa usafiri. Inafikia hatua mpaka viongozi wa uhamiaji wanakimbizana na raia wa kigeni kwa kutumia pikipiki ambayo ni hatari sana kwenye maisha yao. Je, Serikali itapeleka lini gari la Uhamiaji katika Wilaya ya Kahama?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Serikali inaendelea kuimarisha kuviwezesha vyombo vyake vya usalama ili viweze kutekeleza majukumu yake vizuri. Bahati mbaya katika swali la msingi huwa tunauliza polisi na hili limekuja kwa Immigration. Tutafuatilia Idara ya Immigration kuona uwezekano wa kuwapatia watu wa Kahama gari kulingana na changamoto ya wageni na shughuli za kibiashara nyingi zilizopo katika Mji wa Kahama. Kwa hiyo tutawasiliana na Mheshimiwa Mbunge ili kuona namna ya kutanzua tatizo hilo, nashukuru.

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. OMAR ALI OMAR aliuiliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka magari kwa jeshi la polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba?

Supplementary Question 3

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Mwaka 2015 nilipata msaada wa gari la Polisi kutoka Japan, nikalipeleka kwenye Kituo cha Afya cha Gonja ambacho kiko Kata ya Maole. Mimi mwenyewe nilifuatilia, Serikali ilikuwa hailiangalii lile gari mpaka sasa hivi sijui lina hali gani. Je, Waziri ataniambia leo Serikali itakwenda kuliangalia lile gari lirudi barabarani kama nilivyolileta kutoka Japan?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimuahidi Mheshimiwa Malecela Anne Kilango, kwamba binafsi nitalifuatilia kuona hilo gari liko wapi na ni changamoto gani inayosababisha lisiende kuwahudumia watu wa Gonja kama ilivyokusudiwa na Mheshimiwa Mbunge katika jitihada zake za kutafuta gari hilo. Namuahidi Mheshimiwa nitalifuatilia kwa kina baada ya kikao hiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. OMAR ALI OMAR aliuiliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka magari kwa jeshi la polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba?

Supplementary Question 4

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Katika wilaya ya Kilwa Jeshi letu la Polisi lina gari chakavu sana. Je, ni lini Serikali itapeleka gari jipya kwa ajili ya matumizi ya Jeshi letu la Polisi, Wilayani Kilwa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema kwenye jibu langu la msingi kwamba katika mwaka huu wa bajeti tunaoendelea nao, Serikali imetutengea bilioni 15 kwa ajili ya ununuzi wa magari na ahadi yetu ni kwamba ma-OCD wote watapata mgao wa magari haya. Kwa hiyo, Mheshimiwa Ndulane kule Kilwa pia watapata mgawo wao, nashukuru.

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. OMAR ALI OMAR aliuiliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka magari kwa jeshi la polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba?

Supplementary Question 5

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Je, Serikali itapeleka lini magari katika Mkoa wa Kusini, Pemba ambao una uhaba wa magari hayo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kurejea jibu langu la msingi kwamba, mara tutakapopokea magari yatakayonunuliwa kwa bilioni 15 tulizopewa na Serikali ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Mkoa wa Kusini Pemba pia ni moja ya maeneo yatakayogawiwa magari hayo. Namwondoa mashaka Mheshimiwa Maida kwamba Mkoa wake pia utapata gari, ahsante.