Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 17 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 221 2023-05-03

Name

Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE K.n.y. MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Mahakama ya Ardhi chini ya Muhimili wa Mahakama?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Njalu Daudi Silanga, Mbunge wa Itilima kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumo wa utatuzi wa migogoro ya ardhi unaanzia katika ngazi ya Mabaraza ya Ardhi ya Vijiji na Mabaraza ya Kata ambayo yote yana mamlaka ya kufanya usuluhishi. Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya ndiyo yenye jukumu la kutatua migogoro ya ardhi nchini ambapo ikiwa mtu hakuridhika na uamuzi wa Baraza la Ardhi na Nyumba ya Wilaya atakata rufaa kwenda Mahakama Kuu au Mahakama ya Rufani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uwepo wa Mahakama ya Ardhi napenda kumfahmisha Mheshimiwa Mbunge kuwa katika Mahakama Kuu kuna Divisheni maalum ya Mahakama Kuu, Kitengo cha Ardhi. Hata hivyo, Serikali inaendelea kufanya maboresho katika Marabaza ya Ardhi ili kuangalia namna bora ya kuyawezesha ikibidi ihamishiwe katika Muhimili wa Mahakama, ahsante.