Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 21 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 264 2023-05-09

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza: -

Je, Serikali imejipanga vipi kushughulikia malalamiko kuhusu kikototoo?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jesca Jonathan Msambatavangu, Mbunge wa Iringa Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilitangaza matumizi ya kanuni mpya ya mafao ya kikokotoo ya pensheni kuanzia tarehe 1 Julai, 2022 kupitia Gazeti la Serikali Na. 357 Toleo la Tarehe 20 Mei, 2022. Kanuni hiyo iliandaliwa kwa kuzingatia haja ya kuboresha, kuwianisha mafao ya wanachama na kuifanya Mifuko ya Pensheni kuwa endelevu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua wajibu wa kuwaelimisha wananchi hususan waajiri na wanachama wa Mifuko ya Pensheni kuhusu Kanuni mpya ya Mafao ya Pensheni, elimu imeendelea kutolewa na Mifuko ya Pensheni kwa kushirikiana na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA). Hadi kufikia tarehe 28 Februari, 2022, Mifuko iliweza kutoa elimu kwa jumla ya waajiri 2,927 (PSSSF), waajiriwa 318 na NSSF waajiriwa 2,609 ambapo wanachama 71,836 wa PSSSF wakiwa 19,656 na NSSF 52,180 walifikiwa na mafunzo hayo. Mifuko inaendelea kutoa elimu kama sehemu ya majukumu yao ya kila siku, ahsante.