Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 21 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 266 2023-05-09

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamalizia Vituo vya Afya Kizengi, Tura, Lutende na Goweko kwa kujenga OPD na kupeleka vifaa tiba?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Jimbo la Igalula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa Vituo vya Afya katika kata za kimkakati ili kusogeza huduma za afya karibu na wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2019/2020 Serikali ilitenga shilingi milioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Lutende katika Halmashauri ya Wilaya ya Uyui. Aidha, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali ilitenga shilingi milioni 300 kwa ajili ya ukamilishaji wa Kituo cha Afya Lutende.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi na ukamilishaji wa vituo vya afya vya kimkakati kote nchini ikiwemo ukamilishaji wa Kituo cha Afya Lutende, na Tura, pamoja na ujenzi wa vituo vya afya katika Kata ya Goweke na Kizengi.