Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia Vituo vya Afya Kizengi, Tura, Lutende na Goweko kwa kujenga OPD na kupeleka vifaa tiba?

Supplementary Question 1

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, Kata ya Lutende ambayo unasema mmetenga shilingi milioni 300 ambayo itaenda kumalizia kituo cha afya, fedha hiyo haijaenda mpaka siku ya leo; je, ni lini fedha hiyo itakwenda kumalizia Kituo cha Afya cha Kata ya Lutende?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Wananchi wa Kata ya Igalula wamejenga boma la wodi ya kulazia wagonjwa na Serikali imeleta fedha nyingi na tumenunua vitanda, hakuna sehemu ya kuvipeleka; je, Serikali haioni haja ya kupeleka fedha kumalizia wodi hiyo kwa sababu operation mpaka sasa hivi ni 27 hakuna sehemu ya kuwalaza? Nakushukuru.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Venant, la kwanza fedha hii shilingi milioni 300 katika Kituo cha Afya Lutende, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi kwamba ilikuwa ni kwenye mwaka wa fedha ambao umepita, sasa nitakaa na Mheshimiwa Mbunge tuweze kuona nini kilitokea hata fedha hii mpaka sasa haijafika, na kama kuna mkwamo wowote, basi tutashirikiana kwa pamoja kuhakikisha kwamba fedha hii inafika katika Kituo cha Afya cha Lutende.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili la Igalula, fedha ya kukamilisha wodi. Serikali itaendelea kutoa fedha kadiri ya upatikanaji ili kukamilisha majengo mbalimbali kwenye vituo vya afya, zahanati na hospitali za wilaya kote nchini. Kwa hiyo, fedha itakapopatikana, basi tutahakikisha Kituo cha Afya Igalula nacho kinapata fedha.