Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 21 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 267 2023-05-09

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE.SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga barabara ya Mureru – Diloda – Gorimba – Masusu hadi Waama ili ipitike wakati wote?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Samweli Hhayuma, Mbunge wa Hanang, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Mureru – Diloda – Gorimba – Masusu hadi Waama imegawanyika katika vipande viwili vya Mureru – Waama chenye urefu wa kilometa 34 na Diloda – Gisambalang’ chenye urefu wa kilometa 25.1.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2022/2023, TARURA imefungua kipande cha barabara ya Mureru - Waama kwa kiwango cha tabaka la udongo yenye urefu wa kilomita 34 na ujenzi wa (culvert) yaani vivuko 11 vya maji kwa gharama ya shilingi milioni 284.99. Awali kipande hiki kilikuwa ni njia ya ng’ombe (Pario). Aidha, katika mwaka wa fedha 2023/2024, shilingi milioni 80 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa culvert, yaani vivuko 16 vya maji katika barabara hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ufunguzi wa kipande cha barabara ya Diloda – Gisambalang’ chenye urefu wa kilometa 25.1 utafanyika kadiri ya upatikanaji wa fedha ambapo kwa sasa kinatumika kama njia ya ng’ombe (pario).