Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE.SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga barabara ya Mureru – Diloda – Gorimba – Masusu hadi Waama ili ipitike wakati wote?

Supplementary Question 1

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, hii barabara ili ilete tija inayokusudiwa, ni muhimu kufungua barabara ya Mashaw - Waranga, barabara ya Masusu – Gisambalang – Mhanda; je, Serikali iko tayari kutenga fedha haraka ili barabara ziweze kufunguliwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Wilaya ya Hanang’ ina maeneo mengi ambapo mvua ikinyesha yanakuwa kama kisiwa. Mfano Mara, Uteshi, Merekwa, Gaulol, Ghetaghul na Gijetamogh; je, Serikali haioni ni wakati muafaka sasa kuingozea TARURA Wilaya ya Hanang’ bajeti?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza; la kwanza, hii barabara ambayo ameitaja ya Marang, Masusu, Gisambalang na maeneo ya kule Hanang’ Serikali itaendelea kutenga fedha kadiri ya upatikanaji wa fedha hizi. Vile vile kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, barabara hii ilikuwa ni ya kupita mifugo (Pario). Kwa jitihada kubwa za Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na TARURA kuongezewa fedha, imeanza kufunguliwa na sasa zaidi ya kilometa 30 tayari zimetengenezwa na kadiri miaka inavyokwenda tutazidi kuhakikisha barabara hii inafunguliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili la barabara hii za Katesh, Berekwa na maeneo yale ya kule Hanang ambayo ameyataja Mheshimiwa Hhayuma, TARURA kwa mwaka wa fedha huu unaomalizika ilitengewa shilingi bilioni 2.33 kwa Wilaya ya Hanang peke yake. Hii ni zaidi ya mara tatu ya bajeti ambayo ilikuwa 2020/2021 ya barabara katika Wilaya ya Hanang’. Hivyo Mheshimiwa Mbunge awe tu imani kwamba katika bajeti inayofuata hii, vilevile TARURA wametengewa bajeti hiyo hiyo ya shilingi bilioni 2.33 kule Wilaya ya Hanang na barabara nyingi zitafunguliwa kuhakikisha kwamba wananchi wake kule wanapita bila matatizo yoyote.