Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 21 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 268 2023-05-09

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga shule ya msingi ya watoto wenye mahitaji maalum katika Halmashauri ya Morogoro?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Edward Kalogeris, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Halmashauri ya Morogoro ina watoto wenye mahitaji maalum. Hadi sasa halmashauri imeanza kujenga bweni kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalum katika shule ya msingi Mvuha. Shule hii ina jumla ya wanafunzi 24, Serikali tayari imekwishapeleka kiasi cha shilingi milioni 100 katika shule hii katika mwaka wa fedha 2022/2023 kwa ajili ya ujenzi wa bweni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga na kupeleka fedha katika Halmashauri ya Morogoro kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha.