Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga shule ya msingi ya watoto wenye mahitaji maalum katika Halmashauri ya Morogoro?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali pamoja na kupeleka fedha ile shilingi milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni na kazi inaendelea bado kuna uhitaji wa walimu pindi kazi itakapokuwa imekamilika. Vilevile kuna uhitaji wa uzio ili kuweza kuweka usalama kwa watoto hao wenye mahitaji maalum. Je Serikali ina mpango gani wa kupeleka fedha hizo na walimu pindi kazi itakapokamilika? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; je, Mheshimiwa Naibu Waziri uko tayari kufanya ziara katika Jimbo la Morogoro Kusini na kuandamana na mimi ili kwenda kuangalia mahitaji mengine ya elimu na afya katika halmashauri yetu? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijajibu maswali yake haya mawili kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge Mheshimiwa Kalogeris kwa sababu jambo hili ni wiki iliyopita tu alikuja kulifatilia pale ofisini kuhakikisha kwamba wanapata walimu. Nimuhakikishie mbele ya Bunge lako Tukufu nikijibu swali lake la kwanza kwamba katika ajira hizi ambazo zimetolewa kibali na Mheshimiwa Rais kuweza kuajiri tutahakikisha shule hii kwa sababu ni watoto wenye mahitaji maalum wanapata walimu wa kuweza kuwafundisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili nipo tayari kuongozana na Mheshimiwa Mbunge mpaka kwenda Jimbo Lake la Morogoro Kusini kwenda kuitembelea shule hii na tuone ni nini kinaweza kikafanyika na Serikali kwa ajili ya kujenga uzio ambao ameuzungumzia Mheshimiwa Mbunge pale.