Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 21 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 269 2023-05-09

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza: -

Je, ni kwa nini skimu za umwagiliaji za Liyuni na Limamu – Namtumbo hazijakamiliki ingawa Serikali imetumia fedha nyingi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, skimu ya umwagiliaji ya Mtakuja iliyopo katika Kata ya Limamu yenye ukubwa wa eneo la hekta 350 na Liyuni iliyopo katika Kata ya Mchomoro yenye ukubwa wa hekta 140 ni miongoni mwa skimu zilizopo katika Wilaya ya Namtumbo. Katika mwaka 2006/2007 hadi 2012/2013, Serikali iliwekeza kiasi cha shilingi bilioni 1.260 kwa ajili ya ujenzi wa mfereji mkuu mita 3,950, vivuko viwili, daraja moja, kalvati na barabara yenye urefu wa kilomita 25 katika mradi wa Liyuni na ujenzi wa banio, mfereji mkuu mita 3,000 vivuko katika skimu ya Mtakuja kupitia fedha za DADPs, DIDF na MIVARF.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa usanifu wa skimu hizi ulifanyika muda mrefu, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji katika mwaka wa fedha 2023/2024 imepanga kufanya mapitio ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili kubaini gharama halisi za kukamilisha miundombinu ya umwagiliaji na kuhakikisha skimu hiyo inakamiliaka na kuleta tija ya kilimo cha umwagiliaji katika kata za Limamu na Mchomoro.