Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza: - Je, ni kwa nini skimu za umwagiliaji za Liyuni na Limamu – Namtumbo hazijakamiliki ingawa Serikali imetumia fedha nyingi?

Supplementary Question 1

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa maeneo haya yana jumla ya hekta zaidi ya 490 na Serikali iliwekeza kama ilivyosema bilioni 1.260 lakini sasa maeneo haya imekuwa wafugaji wanafanya kama maeneo ya malisho na kuharibu mazingira katika maeneo yale. Je, Serikali inaweza kuharakisha kazi iliyokusudia ili kumaliza miundombinu yake na kuweza kufanya kazi ya kilimo cha umwagiliaji kiweze kuendele kwa mwaka mzima?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Serikali kuu inaweza kutusaidia kuondoa wafugaji hawa katika maeneo yale ili yabaki kama eneo la kilimo kama lilivyokusudiwa na kwa kuwa Serikali iliwekeza fedha nyingi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa Mbunge wa Namtumbo kama ifuatanvyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali la kwanza la kuharakisha nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika miradi ambayo tuliipitia nchi nzima na kuangalia hatua ambayo imefikia na imekwamia wapi ni pamoja na miradi hii ambayo ipo Kata za Liyuni na Limamu nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, kwamba katika mwaka huu wa fedha tutahakikisha kwamba tunafanya upembuzi yakinifu ili kazi ya ujenzi ianze mara moja na wananchi waanze kufanya kilimo cha umwagiliaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ya kuhusu wanyama, hili liko ndani ya Uongozi wa wilaya husika na sisi tuko tayari kusaidia nao kuhakikisha kwamba eneo hili linalindwa hivyo nitoe rai kwa uongozi wa Wilaya kuhakikisha kwamba maeneo haya yanasimamiwa vizuri na yanalindwa ili yabaki katika matumizi ambayo yamekusudiwa. (Makofi)