Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 21 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 270 2023-05-09

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: -

Je, ni lini Wakulima wa Tumbaku watalipwa fedha zao kutoka Kampuni ya JESPAN ya msimu wa mauzo 2021 Jimboni Muhambwe?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Florence George Samizi Mbunge wa Muhambwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika msimu wa mwaka 2020/2021, kampuni ya JESPAN Company Limited ilinunua jumla ya kilo 512,426 za tumbaku zenye thamani ya Dola za Marekani 662,651. Kampuni hiyo iliweza kulipa wakulima wa Kibondo, Kakonko na Kasulu kiasi cha Dola za Marekani 471,500 na kubaki deni la kiasi cha Dola za Marekani 191,151.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na ucheleweshwaji wa malipo, Serikali imeanza kuchukua hatua za kisheria kwa kampuni zilizonunua tumbaku kwa wakulima na kushindwa kufanya malipo. Hivyo basi, malipo ya wakulima yatafanywa kwa mujibu wa maamuzi ya vyombo vya haki ikiwemo Mahakama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kampuni hiyo iliyoshindwa kulipa wakulima baada ya soko la kuuza tumbaku iliyonunua kuyumba na kutouza kutokana na athari za UVIKO – 19. Aidha, Wizara kupitia Bodi ya Tumbaku na Chama Kikuu cha Wakulima wa Tumbaku Mkoa wa Kigoma (KTCU) na Ofisi ya Mashtaka ya Mkoa wa Kigoma inakamilisha taarifa za kuifungulia kesi ya madai kampuni ya JESPAN Company Limited ili kukamilisha malipo ya wakulima.