Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: - Je, ni lini Wakulima wa Tumbaku watalipwa fedha zao kutoka Kampuni ya JESPAN ya msimu wa mauzo 2021 Jimboni Muhambwe?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naishukuru sana Serikali kwa majibu hayo mazuri pamoja na majibu hayo mazuri bado nina maswali ya nyongeza. Wahanga waliozulumiwa pesa zao katika Jimbo la Muhambwe ni Lugongwe AMCOS, Chapakazi AMCOS, Amani AMCOS na Migwezi AMCOS ambao hawa waliingia mikataba na JESPAN baada ya kuwa wamejiridhisha kwamba Serikali imewapatia vibali hawa JESPAN.

Je, Serikali aioni iko ukunimu wa kulipa hizi pesa kwa sababu wao ndiyo waliyowadhamini hawa wakulima halafu wenyewe Serikali itaendelea na hizo kesi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa makampuni haya ya wazawa yanawazulumu hawa wakulima hii JESPAN ni mfano tu. Serikali imejipanga vipi kuyadhibiti haya makampuni ili wakulima wetu wasiendelee kudhulumiwa? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli makampuni haya tumeanza kuchukua hatua za kisheria, baadhi ya makampuni yanatoa huduma kwenye sekta ya tumbaku baadhi yao tumeishayakata fedha kupitia TCJE kama dola lakini nne ambazo walitoa huduma ili tuweze kuzirudisha kwa wakulima. lakini hatua ya pili ni kwamba Serikali inapompa leseni kwenda kufanya biashara anapokwenda kinyume kuna utaratibu wa kisheria na kwake yeye kupewa leseni ya kwenda kufanya biashara haina maana ile responsibility siku ya mwisho itahamia kwa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tabia ya wakulima kudhulumiwa na wafanyabiashara na hii haipo tu kwenye tumbaku, ipo kwenye pamba, ipo kwenye korosho, ipo kwenye maeneo mengi, na wizi mwingine hushirikisha vyama vya ushirika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano kesi iliyoko Mkoa wa Katavi chama cha ushirika kimeshirikiana na Kampuni ya NEIL kuweza kuwaibia wakulima. Kwa hiyo, tunachukua hatua za kisheria niwaombe Waheshimiwa Wabunge wa Sikonge Wilaya ya Sikonge Mkoa wa Katavi, Mkoa wa Tabora na Wilaya ya Chunya wa tumbaku waliyopata madhara mwaka 2019/2020 niwahakikishie kwamba Serikali inachukua hatua na tutamaliza haya matatizo na yamekuwa fundisho kwetu ndiyo maana tumewaondoa wanunuzi wa namna hii na tunakuja na sheria ya kilimo itakayoweza ku–criminalize wizi unaofanyika kwenye sekta ya kilimo. (Makofi)