Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 21 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 272 2023-05-09

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALOME W. MAKAMBA K.n.y. MHE. FELISTA D. NJAU
aliuliza: -

Je, nini mkakati wa Serikali wa kupunguza msongamano wa wafungwa magerezani?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Felista Deogratius Njau, Mbunge wa Viti maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika magereza yetu upo msongamano mkubwa unaosabishwa na idadi kubwa ya mahabusu kuliko wafungwa hususani katika magereza ya mijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jitihada zinazochukuliwa na Serikali kupunguza msongamano wa wafungwa magerezani, ni pamoja na kuhimiza matumizi ya vifungo vya nje kama vile Parole, Extra Mural Labour, huduma kwa jamii na huduma za uangalizi kwa wafungwa wenye viashiria vya kujirekebisha, msamaha unaotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika maadhimisho ya sherehe za Muungano wa Tanzania na Uhuru wa Tanzania Bara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkakati wa Serikali ni kuendelea kuelimisha na kuhimiza wananchi waishi kwa maadili bora na waepuke kuvunja sheria ili waepuke kufikishwa mahakamani na kufungwa. Aidha, Serikali itaendeleza mpango wa kujenga magereza mapya na kufanya upanuzi kwa magereza ya zamani ili kuongeza nafasi ya kuwahifadhi wafungwa na mahabusu kulingana na mahitaji na kutegemea upatikanaji wa fedha, ahsante.