Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALOME W. MAKAMBA K.n.y. MHE. FELISTA D. NJAU aliuliza: - Je, nini mkakati wa Serikali wa kupunguza msongamano wa wafungwa magerezani?

Supplementary Question 1

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru pamoja na majibu ya Serikali ninayo maswali mawili ya nyongeza. Swali langu la kwanza juzi wakati Mheshimiwa Naibu Waziri anajibu swali linalofanana na hili alieleza bayana kwamba mahabusu wengi wanashindwa kutoka, kwa sababu ndugu zao au jamaa hawaendi kuwawekea dhamana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu yapo makosa ambayo mtu anaweza akajidhamini mwenyewe na hili litapunguza msongamano mkubwa kwenye magereza. Nini kauli ya Serikali kwa Jeshi la Polisi na Magereza ambao mpaka sasa hivi wanaweka vikwazo kwa mtu kujidhamini mwenyewe na kuweza kutoka katika vizuizi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; bado katika magereza yetu njia zinazotumika kufanya ukaguzi kwa wafungwa hasa wanawake zinawadhalilisha wanawake na zinawaondolea utu wao na kuvunja haki zao. Kwa nini Serikali inashindwa kununua vifaa vya kisasa vya kufanya ukaguzi ili kuweza kutunza staha za wafungwa na maabusu hasa wanawake? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba masuala ya dhamana yapo ya namna mbili moja inaweza kutolewa na polisi na nyingine inatolewa na Mahakama. Sasa pale ambapo kuna changamoto za polisi juzi nilieleza kwamba tunawahimiza RPC’S, OCD’S na Wakuu wa vituo wazingatie sheria kila inapotokea kosa inastahili dhamana watu waweze kutoa dhamana lakini pale inaposhindikana Mahakama ikitoa amri mtu apewe dhamana always tuta–comply ili dhamana iweze kutolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu upekuzi unaodhalilisha tunatambua hilo na ndiyo maana kwenye bajeti yetu ijayo tumetenga fedha kwa ajili ya kununua vifaa vya kisasa vya kiteknolojia kuepusha ukaguzi unaodhalilisha siyo wanawake tu hata wanaume pia ili mtu akishapita pale anaonekana kama alivyo salama basi itakuwa imekamilika, ahsante.