Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 21 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 274 2023-05-09

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: -

Je, kuna mpango gani kufanya utafiti na kurasimisha pombe ya mwiki inayotokana na mabibo ili kuongeza thamani ya zao la korosho?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara napenda kujibu swali la Mheshimiwa Agnes Elias Hokororo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na changamoto kadhaa zinazowakabili wazalishaji wa pombe za kienyeji hivyo kushindwa kukidhi matakwa ya viwango na kukosa ithibati ya ubora, Serikali kupitia Shirika la Viwago Tanzania (TBS) pamoja na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) imeweka utaratibu wa kutoa mafunzo kwa wazalishaji wa pombe za kienyeji kuhusu matumizi ya teknolojia bora na matumizi sahihi ya viwango katika kuzalisha pombe za kienyeji ikiwemo pombe aina ya mwiki ili ziweze kukidhi viwango vinavyokubalika na hivyo kuruhusiwa kuingia sokoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi kufikia mwezi Oktoba, 2022, jumla ya leseni 43 za ubora zimetolewa kwa bidhaa mbalimbali za pombe za kienyeji, na maombi mengine mapya 22 yapo kwenye hatua mbalimbali za tathimini kuelekea kwenye kupata ithibati ya ubora. Aidha, Serikali kupitia Shirika la Viwango Tanzania itaendelea kutengeneza viwango vya pombe za kienyeji kwa kadri mahitaji yatakavyojitokeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.