Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: - Je, kuna mpango gani kufanya utafiti na kurasimisha pombe ya mwiki inayotokana na mabibo ili kuongeza thamani ya zao la korosho?

Supplementary Question 1

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru lakini sio mwiki ni mvuke. Maswali mawili ya nyongeza: -

a) Je, kwa nini SIDO na TBS isijielekeze katika kuboresha teknolojia za asili za watengenezaji wa pombe ya mvuke ya mabibo badala ya kuendelea kutoa mafunzo?

b) Je, kwa nini Serikali, isipitie watengenezaji wote wa pombe ya mabibo, badala ya kusubiri waombaji wachache wenye uwezo wa kuagiza mitambo kwa ajili ya kupata hizo ithibati za TBS na SIDO?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ni kweli kabisa kwanza nimpongeze Mheshimiwa Agnes Hokororo kwa kuleta tena hili swali ambalo ni hoja muhimu sana kwa Watanzania wengi ambao wengi tumeendesha shughuli zetu za kusoma shule na mambo mengine kupitia pombe hizi za kienyeji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, kweli tunachofanya sasa ni kuboresha teknolojia zilizopo lakini pia kuna wakati mwingine tungependa kupata teknolojia rahisi lakini za kisasa zaidi. Ndiyo maana SIDO tunahakikisha tunawatembelea wazalishaji hawa na kuwasaidia. Kama ambavyo nimesema, tayari kuna haya maombi, maana yake hawa ni wale ambao wana uwezo wa kuomba; lakini ambao sasa hawana uwezo wa kuomba, kama ambavyo nimesema wale wazalishaji wa pombe hii ya mvuke kupitia mabibo, tumeshaamua sasa tutawatembelea wauzaji wote wa pombe za kienyeji ili tuwaelimishe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, tutawaelimisha kuhusu mazingira sahihi ya kuzalishia, kwa maana ya kuzalisha pombe, ambapo itakuwa na mazingira sahihi mazuri. Pili tuwasaidie teknolojia rahisi na kuzihuisha zile zilizopo ili ziwe katika mazingira ambayo yatapelekea kupata viwango sahihi vya pombe. Tatu, tuwasaidie kuhakikisha wanapata teknolojia ya kutunza, packaging ili zile pombe zisiharibike mapema au zipate shida ambayo itapelekea kuwa sumu kwa walaji katika mazingira mabayo si sahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.