Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 21 Energy and Minerals Wizara ya Madini 276 2023-05-09

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: -

Je ni lini Serikali itafungua Ofisi ya Madini Liwale?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI K.n.y. WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka, Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, uanzishwaji wa ofisi ya madini unazingatia vigezo mbalimbali ikiwemo uwepo wa shughuli kubwa za madini katika eneo husika. Kigezo hiki kinalenga katika kuhakikisha kunakuwa na usimamizi na udhibiti madhubuti wa rasilimali madini inayoanzishwa katika eneo husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Mkoa wa Lindi, pamoja na kuwa na Ofisi ya Madini ya Mkoa iliyopo Nachingwea pia Wizara imefungua ofisi ndogo iliyopo Lindi Mjini ili kurahisisha uratibu wa shughulil za madini katika maeneo mengine katika mkoa huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shughuli za uchimbaji katika Wilaya ya Liwale zipo chini ukilinganisha na Wilaya za Ruangwa, Kilwa na Nachingwea. Kwa sasa wachimbaji wa madini katika Wilaya ya Liwale wanashauriwa kutumia Ofisi ya Afisa Madini Mkazi ya Nachingwea pamoja na ofisi ndogo ya madini iliyopo Lindi Mjini. Hata hivyo, Wizara itaendelea kuboresha huduma kwa wadau wake kwa kadiri itakavyopata fedha za kutekeleza jukumu hilo.