Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 21 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 277 2023-05-09

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kuwa vyuo vikuu vyenye taaluma ya sayansi na tiba vinakuwa na hospitali za kufundishia?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKINOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Thea Medard Ntara Mbunge wa Viti Maalaum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mitaala ya Mafunzo ya Sayansi ya Utabibu (Medical and Health Training) vyuoni hutekelezwa kwa mafunzo ya nadharia na vitendo ambavyo hufanyika katika hospitali zenye wagonjwa halisi. Kwa vyuo ambavyo havina hospitali za mafunzo kwa vitendo, upo utaratibu wa makubaliano kati ya vyuo na hospitali za rufaa, mikoa, wilaya pamoja hospitali za watu binafsi zenye kukidhi vigezo kwa ajili ya kuwawezesha wanafunzi wanaosoma katika vyuo hivyo kufanya mafunzo kwa vitendo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa vyuo vikuu vyenye taaluma ya sayansi na tiba kuwa na hospitali za kufundishia; ambapo kwa sasa inaendelea na ujenzi wa Hosipitali ya Mloganzila kama hospitali ya kufundishia ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili. Aidha, Serikali itaendelea kutafuta vyanzo mbalimbali vya fedha kwa ajili ya kujenga hospitali za kufundishia katika vyuo vikuu vingine vyenye taaluma ya sayansi na tiba ambavyo havina hospitali hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.